Watu 7 zaidi wapatikana na virusi vya corona

August 2024 ยท 2 minute read

Idadi ya watu wanaougua virusi vya corona inazidi kuongezeka nchini Kenya huku saba wakipatikana na maradhi hayo Aprili 8.

Idadi ya walioambukizwa coronavirus nchini Kenya kufikia sasa ni watu 179.

Habari Nyingine: Mkurugenzi mkuu wa twitter achanga KSh 100 bn kupigana na coronavirus

Akiongea Jumatano, Aprili 8, Katibu Msimamizi katika wizara ya Afya daktari Mercy Mwangangi alisema saba hao ni Wakenya.

Aliongeza kuwa watatu kati yao ni watoto walio chini ya miaka 15.

Habari Nyingine: Polo ataka mke anyoe akidai saluni ni ghali

Nairobi inaendelea kuongoza katika maambukizi ya coronavirus kwani watano kati ya saba hao ni kutoka jijini.

Mmoja ni kutoka Mombasa na mwingine ni kutoka kaunti ya Uasin Gishu.

Matokeo hayo yalipatikana baada ya watu 305 kupimwa ndani ya masaa 24 yaliyopita.

Habari Nyingine: Saburi afungwe kwa miaka 10 gerezani, apendekeza Rais Uhuru

Tangazo la wizara ya Afya lilijiri wakati ambapo Wakenya waliamkia taarifa za kuwa wabunge 17 wana virusi vya covid-19.

Taarifa hizo zilizua tumbo joto huku baadhi ya wabunge wakijitokeza na kupinga madai hayo

Coronavirus imekuwa tishio kubwa la kiafya ulimwenguni huku Kenya ikiwa imepoteza watu wanne kutokana na maradhi hayo.

Wengine wanne nao waliripotiwa kupona akiwemo aliyekuwa mgonjwa wa kwanza humu nchini Brenda Ivy.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsaApp: 0732482690.

Subscribe to watch new videos

Chanzo: TUKO.co.ke

ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2Bvzmeinmdjan12f5JmrpqspWKEbsbAopuiZaeWvaLAyKSYp5ldo65uwsirrKyhXavGonnCqKmoppFjtbW5yw%3D%3D